Thursday, January 22, 2015

Late Post: Mkutano Mkuu wa Baraza la Watoto Tanzania.....

Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni chombo cha kuwashirikisha watoto katika maamuzi mbalimbali ya kitaifa na kimataifa. Baraza la Watoto lilianzishwa mwaka 2002 likiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa watoto katika ngazi mbalimbali za jamii kama  mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto (CRC) ulivyoeleza ambapo Tanzania kama nchi mwanachama wa Umoja wa mataifa unapaswa kuutekeleza.

kila baada ya miaka 2 Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hufanya mabadiliko ya uongozi katika kuliendesha Baraza la watoto la Jamhuri ya Muungano wa Tanzanaia na mwaka huu uchaguzi utafanyika tarehe 21 Januari 2015 baada ya ule wa mwaka 2013.


http://michuzi-matukio.blogspot.com/2015/01/mkutano-mkuu-wa-baraza-la-watoto-wa.html#links

Tuwawezeshe watoto kupanga maisha yao ya baadaye, kuwa wabunifu na kupata Elimu.

No comments: